Jumatano, 23 Novemba 2016

PROF. MBARAWA KUMUWAKILISHA RAIS MAGUFULI MKUTANO WA USAFIRISHAJI DUNIANI



Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa atamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika mkutano wa kimataifa wa Usafirishaji Duniani utakaofanyika katika mji wa Ashgabat nchini Turkemistan kuanzia tarehe 26-27 Novemba, 2016.

Ajenda kuu ya mkutano huo ulioitishwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambao utashirikisha viongozi mbalimbali utajadili kwa kina maeneo muhimu ya ushirikiano wa kimataifa kwenye Sekta ya Usafirishaji kwa maendeleo endelevu Duniani.

Aidha katika mkutano huo Waziri Prof. Mbarawa atapata fursa ya kukutana na wawekezaji mbalimbali Duniani waliobobea katika sekta ya usafirishaji na kuwashawishi kuwekeza hapa nchini. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni