Alhamisi, 27 Aprili 2017

Hotuba ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa mwaka wa Fedha 2017-2018



HOTUBA YA WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO MHESHIMIWA PROF. MAKAME M. MBARAWA  (MB), ILIYOWASILISHWA BUNGENI MPANGO NA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA  MWAKA WA FEDHA 2017/2018


http://www.mwtc.go.tz/uploads/publications/en1493281737-HOTUBA%20WUUM%202017-2018.pdf

Ijumaa, 21 Aprili 2017

WATUMISHI SEKTA YA UJENZI WAPEWA SOMO


Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga (Wa pili kulia), akizungumza na wafanyakazi wa Wizara hiyo pamoja na wawakilishi kutoka Taasisi zilizo chini ya Wizara katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi, Mkoani Morogoro.



Katibu wa Baraza la Wafanyakazi (Sekta ya Ujenzi), Bw. Ramadhani Msafiri(Wa pili kushoto), akifafanua jambo kwa wafanyakazi wa Wizara hiyo pamoja na Wawakilishi kutoka Taasisi zilizo chini ya Wizara katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi, Mkoani Morogoro.


Mmoja wa wafanyakazi wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Bw. Shukuru Sikunjema, akitoa maoni yake kwa Mwenyekiti Wa Baraza la Wafanyakazi Eng. Joseph Nyamhanga katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi, Mkoani Morogoro.


Wafanyakazi wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) wakifuatilia maelekezo ya Baraza la Wafanyakazi wakati wa kikao hicho kilichofanyika Mkoani Morogoro.


Wafanyakazi wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Wakiimba nyimbo ya ‘Solidarity forever’ kuonyesha mshikamano katika utendaji kazi wakati wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi, Mkoani Morogoro.


Wafanyakazi wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufunga kikao cha Baraza la Wafanyakazi kilichofanyika Mkoani Morogoro.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng.Joseph Nyamhanga, amewataka watumishi wa Wizara hiyo kutekeleza majukumu yao kwa  weledi na uadilifu ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya Serikali ya Awamu ya Tano.

Akisoma hotuba ya ufunguzi kwa niaba ya Waziri wa Wizara hiyo Profesa Makame Mbarawa, katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi leo, mkoani Morogoro, Eng. Nyamhanga, ametoa wito kwa watumishi wote kushirikiana kwa pamoja katika kutekeleza majukumu yao ili kuleta tija kwa Serikali na Taifa kwa ujumla.

"Naliomba baraza hili la wafanyakazi kuhakikisha linahamasisha watumishi wote wa Wizara kutekeleza majukumu yao  kwa kuzingatia maadili, weledi na ushirikiano ili kuleta ufanisi", amesema Eng.Nyamhanga.

Aidha, Eng. Nyamhanga amelisisitiza Baraza hilo kuandaa mkataba wa kupima utendaji kazi wa watumishi katika majukumu yao ya kila siku ili kupima ufanisi wa watumishi hao kuanzia ngazi ya juu hadi ya chini.

Katibu Mkuu Nyamhanga, amelitaka  Baraza hilo kuweka mazingira maalum kwa watumishi ikiwemo kuandaa mpango wa mafunzo ya ndani na nje ya nchi ili kuongeza ujuzi kwa watumishi wa Wizara hiyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi Tawi la Ujenzi Bw. Samuel Mticco,  amemhakikishia Katibu Mkuu huyo kutekeleza maagizo yote yaliyosemwa katika Baraza hilo  ikiwemo la uandaaji wa mkataba wa utendaji kazi kwa watumishi.

Kikao hicho cha siku moja cha Baraza la wafanyakazi la Sekta ya Ujenzi pamoja na mambo mengine kimekubaliana kupunguza matumizi ya fedha za Serikali yasiyo ya lazima pamoja na kupambana na vitendo vya ufisadi na rushwa