Jumatatu, 10 Oktoba 2016

WAZIRI PROF. MBARAWA AKAGUA MIUNDOMBINU MKOANI TABORA

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akizungumza  na mkandarasi wa Kampuni ya China Civil pamoja na viongozi wa Serikali mkoani Tabora wakati akikagua ujenzi wa barabara ya Ndono-Urambo yenye urefu wa KM 52 kuona hatua iliyofikiwa.

Meneja wa Wakala wa Majengo Nchini (TBA), mkoa wa Tabora Qs.Tutu Lusama,   akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa kuhusu hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa nyumba ya Mkuu wa Wilaya ya Urambo Bi Angelina Kwingwa wakati akikagua ujenzi wake.

Muonekano wa Nyumba ya Mkuu wa Wilaya ya Urambo mkoa wa Tabora, ambayo ipo kwenye hatua za mwisho za ujenzi wake

Mkandarasi wa Kampuni ya Chicco kutoka China (kushoto), akitoa taarifa ya ujenzi wa barabara ya Kaliua-Kazilambwa yenye urefu wa KM 56 kwa Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kulia), alipokagua barabara hiyo kuona maendeleo yake.

Mbunge wa Jimbo la Kaliua mkoani Tabora, Mhe. Magdalena Sakaya akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa wakati alipokagua barabara ya Kaliua-Kazilambwa yenye urefu wa KM 56 kuona maendeleo yake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni