Jumatatu, 17 Oktoba 2016

PROF. MBARAWA AFANYA ZIARA MKOANI GEITA


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akitoa maelekezo kwa Mkuu wa Kivuko cha MV. Chato, Eng. Fredinand Mishamo (Wa kwanza kushoto), alipokagua kivuko hicho, wilayani Chato, mkoani Geita.


Fundi wa Kivuko cha Mv Chato kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme Nchini (TEMESA), Bw. Mbondo Jackson, akimweleza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, namna injini ya Kivuko cha MV. Chato inavyotumia mafuta, alipotembelea kivuko hicho, wilayani Chato, Geita.


Muonekano wa Kivuko cha MV Chato kilichopo Wilaya ya Chato mkoani Geita.


Mkuu wa Mkoa wa Geita, Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga, akimuonesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (mwenye shati la blue), ramani inayoonesha mtandao wa barabara za mkoa wa Geita, alipomtembelea Ofisini kwake.


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akisisitiza jambo kwa wafanyakazi wanaofanya kazi kwenye Sekta ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (hawapo pichani), alipoongea nao Mkoani Geita.


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akisalimiana na wafanyakazi wa Sekta ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, mara baada ya kuongea nao Mkoani Geita.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni