Jumatatu, 3 Oktoba 2016

PROF. MBARAWA AITAKA TTCL KUTAFUTA WATEJA


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (kushoto), akiangalia taarifa zinazoingia katika mfumo wa kuhifadhi kumbukumbu alipofanya ziara ya kushtukiza katika Kituo mahiri cha kuhifadhi Kumbukumbu cha Taifa (Internet Data Centre), kilichopo eneo la Kijitonyama jijini Dar es salaam.


Msimamizi wa masuala ya TEHAMA Bw. John Chorai (kulia), akimuonesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (kushoto), namna kifaa cha kurekodia malipo kinavyofanya kazi wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika Kituo mahiri cha kuhifadhi Kumbukumbu cha Taifa (Internet Data Centre), kilichopo eneo la Kijitonyama jijini Dar es salaam.


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (wa pili kulia), akikagua moja ya kifaa cha kuhifadhi Kumbukumbu katika kituo Mahiri cha Internet Data Centre cha Taifa kilichopo eneo la Kijitonyama jijini Dar es salaam.


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (wa kwanza kushoto), akifafanua jambo kwa watumishi wa kituo Mahiri cha kuhifadhi Kumbukumbu cha Taifa (Internet Data Centre), kilichopo eneo la Kijitonyama jijini Dar es salaam wakati alipofanya ziara ya kushtukiza kituoni hapo.


Mwakilishi wa Kibiashara kutoka Ubalozi wa Uingereza anayesimamia nchi ya Tanzania na Kenya Bw. Lord Hollick (wa pili kulia) akifafanua jambo  kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (wa kwanza kulia) wakati alipomtembelea ofisini kwake kuzungumzia masuala ya kuboresha miundombinu nchini. Kushoto ni Balozi wa Uingereza nchini Bi Sarah Cookie.


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa ameitaka Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), kutafuta wateja wa kuhifadhi kumbukumbu zao kwenye Kituo mahiri cha kuhifadhi kumbukumbu cha Taifa (Internet Data Center), jijini Dar es Salaam.


Waziri Prof. Mbarawa pia amemuagiza Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni hiyo kuwa mbunifu na kuanza kufuata wateja ana kwa ana na si kusubiri wateja hao kumfuata ofisini kwake.


Prof. Mbarawa ametoa agizo hilo alipofanya ziara ya kushtukiza katika jengo hilo lililopo eneo la Kijitonyama ambapo ameelezea umuhimu wa kufanya jitihada za haraka kutafuta wateja hao kwa lengo la kuongeza pato cha Taifa.


"Natoa wiki mbili kwa Mkurugenzi wa Masoko kuhakikisha analeta wateja wa kuhifadhi kumbukumbu zao katika kituo hiki, ikishindikana atupishe tutafute watu wanaofaa katika taaluma hiyo", amesema Waziri Prof. Mbarawa.


Prof. Mbarawa amesema kuwa Kituo hicho kimeimarishwa kiusalama kwani kimeunganishwa na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano hivyo wateja wataweza kuchukua taarifa zao kwa  uharaka zaidi.


Ameongeza kuwa masuala yote yanayohusu makubaliano ya kibiashara katika kituo hicho yawekwe kwa njia ya maandishi ili kuweza kuweka kumbukumbu sahihi na ufatiliaji inapohitajika.


Naye Kaimu Mkurugenzi wa TEHAMA wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Eng. Peter Mwasalyanda amemuahidi Waziri Mbarawa kutekeleza yale yote aliyoyaagiza yafanyike ili kuboresha huduma katika kituo hicho.


Katika hatua nyingine Waziri Prof. Mbarawa amekutana na Mwakilishi wa Kibiashara kutoka ubalozi wa Uingereza anayesimamia nchi ya Tanzania na Kenya Bw. Lord Hollick na kuzungumzia masuala mbalimbali ya kuboresha miundombinu nchini.


Kituo mahiri cha Internet Data Centre ni cha kwanza kujengwa katika nchi za ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na asilimia 75 zimetengwa kwa ajili ya kutunza taarifa kutoka sekta binafsi na asilimia 25 itatunza taarifa za Serikali hivyo ni fursa mpya kwa wafanyabiashara na wadau mbalimbali wenye taarifa nyingi kuzihifadhi na kuzitumia wanapozihitaji.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni