Ijumaa, 12 Agosti 2016

RAIS MAGUFULI AZINDUA UJENZI WA DARAJA LA FURAHISHA.


Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Eng. Joseph Nyamhanga kulia akijadiliana jambo na Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Barabara (RFB), Bw. Joseph Haule katikati  na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa barabara nchini Eng. Patrick Mfugale wa kwanza kushoto katika hafla ya uzinduzi wa daraja la watembea kwa miguu lililopo maeneo ya Furahisha jijini Mwanza.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli akizindua mitambo inayojenga daraja la waenda kwa miguu na upanuzi wa Barabara ya Uwanja wa Ndege eneo la Furahisha jijini Mwanza, wa pili kutoka kulia ni Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli na watatu kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Ujenzi Eng. Edwin Ngonyani.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na wafanyakazi wa kampuni ya Nyanza Road Works inayojenga daraja la waenda kwa miguu na upanuzi wa Barabara ya Uwanja wa Ndege eneo la Furahisha jijini Mwanza.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli akipata ufafanuzi wa maendeleo ya ujenzi wa daraja la waenda kwa miguu na upanuzi wa Barabara ya Uwanja wa Ndege eneo la Furahisha jijini Mwanza kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa barabara nchini Eng. Patrick Mfugale, kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bw. John Mongela.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli akihitubia wananchi katika mkutano wa hadhara mara baada ya uzinduzi wa daraja la watembea kwa miguu na upanuzi wa Barabara ya Uwanja wa Ndege eneo la Furahisha jijini Mwanza.

Sehemu ya wananchi wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli alipohutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Furahisha jijini Mwanza.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli ameitaka Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano kuhakikisha kuwa ujenzi wa daraja la watembea kwa miguu na upanuzi wa Barabara ya Makongoro jijini Mwanza unakamilika ifikapo disemba mwaka huu.

Aidha amesema upanuzi wa barabara ya Makongoro uliokuwa ujengwe kati ya Furahisha hadi Pasiansi Km 2.8 sasa utaendelezwa hadi kufikia uwanja wa ndege.

Akizungumza mara baada ya kuweka jiwe la msingi la daraja la watembea kwa miguu na upanuzi wa barabara ya Makongoro Mh. Dkt. Magufuli amesema kasi ya ujenzi wa barabara jijini Mwanza uendane na ujenzi wa uwanja wa ndege ili kuwezesha mkoa wa Mwanza kuwa kitovu cha nchi za maziwa makuu.

“Nakuagiza Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano  uhakikishe kuwa barabara na daraja la watembea kwa miguu Furahisha vinakamilika mwezi desemba na mkandarasi wa uwanja wa ndege anaanza kazi mara moja”. Amesisitiza Rais Dkt. Magufuli.

Amesema nia ya Serikali yake ni kununua meli mbili na kujenga daraja kati ya Kigongo na Busisi ili kuboresha huduma za usafiri katika Ziwa Victoria.

Naye Mtendaji mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Eng. Patrick Mfugale amemtaka mkandarasi anaejenga daraja la waenda kwa miguu na barabara ya Makongoro kuhakikisha ujenzi wake unakamilika kwa wakati na ubora unaotakiwa.

Zaidi ya shilingi bilioni 6.4 zinatarajiwa kutumika katika ujenzi huo utakaopunguza msongamano wa magari na ajali katika barabara ya makongoro jijini Mwanza.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni